Tazama Matokeo Hapa
Download Mitihani
Mchungaji na Mlevi Kimeumana. Soma mpaka Mwisho utajua alicho kisema Huyu mlevi. Pia Kwa Sms za Vichekesho na Mada Pamoja Statu za Vichekesho Buree. Follow me Here @japhary for Daily Jokes 😁.
VITUKO: MCHUNGAJI NA MLEVI KIMEUMANA
MCHUNGAJI: Ulianza lini kunywa bia..?
MLEVI: Miaka 18 iliyopita..!
MCHUNGAJI: “Kwa hiyo kwa siku unatumia zaidi ya 10,000 Tsh..?
MLEVI: “Ndio..!”
MCHUNGAJ: Kama u gekuwa unatunza hiyo pesa 10,000 kwa siku leo hii si ungekuwa na Range Rover..?
MLEV: Samahani, naweza kukuuliza swali..?
MCHUNGAJ: Uliza.!
MLEV: Unakunywa bia..?
MCHUNGAJ: “Hapana!
MLEV: Nionyeshe Range Rover yako..!
MCHUNGAJ: “akasepa”…
FUNZO: Usimsimange mtu kwa udhaifu au Ulevi alio nao, jichunguze wewe kwanza ndo ukosoe wengine.
BONUS JOKE.
Dogo mmoja Alipelekwa Hospitali na baba yake, baada ya vipimo Doctor akawa anamuandikia dawa, baba yake akatoka nje kuongea na Simu. Mtoto akamwinamia Doctor na kusema kwa sauti ya chini:- “Doctor Kwenye dozi ya dawa niandikie na FANTA BARIDII, CHIPS na MISHIKAKI kutwa mara 2 kwa siku 30.”
Mpaka Tunavyo Ongea Mtoto amepelekwa Kwenye Maombi. Ametolewa pale Hospitalini mkukumkuku.
Nijulishe Hapo Chini Kwenye Comment ungependa Vituko kama Hivi, au Kwenye Hivi Vichekesho tuongeze Kipi Tu Punguze Kipi. Nawatakia Tabasamu lenye furaha 😊😊.
Kweli ukisikia Mchungaji na Mlevi Kimeumana ndo hivi. Mda Mwingine Ukitoa Ushauri Hakikisha Wewe Kwanza Upo vizuri. ata biblia imesema. “Toa Kwanza Boriti kwenye jicho lako, ndo utoe Kibanzi kwenye jicho la Jirani yako.” Wale Wayahudi Wenzangu nadhani wamesha jua hichi kifungu kipo Kwenye Agano Lipi.
- 243shares
- Facebook167
- Twitter76
- Gmail
- Copy Link