Watoto wa Siku hizi Wana Mambo Kweli. Soma Hapa ujionee Vituko na Nusu kilicho jiri katika Mkasa Huu wa Msichana mmoja aliye Mdanganya Baba yake.
Kwa Sms za Vichekesho, Mada za Vichekesho, kauli za Kuchekesha na Vichekesho vingine Vingi Wewe ni Follow @japhary
WATOTO WA SIKU HIZI WANA MAMBO KWELI: VITUKO NA NUSU.
Msichana alikuwa amekaa na baba yake kibarazani, mara akamuona Jamaa wake Boyfriend wake akija, yule mvulana alipokaribia tu, yule msichana akamwambai:
- MSICHANA: Umekuja kuchukua kile kitabu chako, kinachoitwa “DADDY AT HOME..?” by Ngozi Okafor.
- MVULANA: Hapana!, Nimekuja kuazima kitabu cha Novel kinaitwa “WHERE SHOULD I WAIT FOR YOU..?” by Ngugi wa Thiongo.
- MSICHANA: Aaah! icho sina ila ninacho kimoja kinaitwa “UNDER THE MANGO TREE” by Chimamanda Adichie.
- MVULANA: Ooh! Vizuri, Basi usisahau kuja nacho kesho kitabu cha Okot p’Bitek kile kinachoitwa “CALL ME IN 5 MINUTES BEFORE” Utakapokuja shule.
- MSICHANA: Usijali, tena nina kitabu kipya kinaitwa “I WON’T LET YOU DOWN” by Chinua Achebe. Baba mtu akawatazamaaaa kisha akasema..
- BABA: Vitabu vyote hivyo, mbona vingi sana, atavisoma vyote kweli..?
- MSICHANA: Ndio Daddy, huyu mvulana hupo smart sana na ana akili ata visoma vyote hivyo.
- BABA: Sawa! Usisahau kumpatie na kile ambacho nimekiweka pale Chini ya meza. kinaitwa ” I’M NOT STUPID, I UNDERSTOOD.” Na kuna kingine nimekiweka juu ya kabati la vyombo, kinaitwa “IF YOU GOT PREGNANT, SCHOOL IS OVER.”
Kweli Watoto Wasiku hizi wanatuona Sisi wazazi wao Tulisoma Chini ya Mbuyu. Wamesahau kuwa na Sisi tulikuwa Vijana kama Wao. Kweli watoto wa Siku Hizi Wana Mambo.
Nijulishe Hapo Chini Kwenye Comment ungependa Vituko kama Hivi, au Kwenye Hichi kichekesho tuongeze Kipi Tu Punguze Kipi.
- 210shares
- Facebook147
- Twitter63
- Gmail
- Copy Link